Wednesday, December 5, 2012

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA) YATOA ZAIDI YA SHILINGI MILION 15 KWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA AJILI YA KUBORESHA MFUMO MPYA WA UTOAJI HUDUMA ZA MATIBABU KWA NJIA YA MAWASILIANO (TELE MEDICINE)

Meneja wa TCRA Kanda ya Nyanda za Juu kusini Deograsias Moyo kwa niaba ya mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania akimkabidhi hundi ya zaidi ya sh milioni 15 mkurugenzi wa hospitali ya rufaa Mbeya eliuter Samnkey 

ZAIDI  ya shilingi million 15 zimetolewa na mamlaka ya mawasiliano Tanzanzania (TCRA)  nyanda za juu kusini   ajiri ya  kuboresha mfumo  mpya wa utoaji  huduma za matibabu kwa njia ya mawasiliano (TELE MEDICINE) ili kupunguza vifo na  gharama za usafiri kwa wagonjwa.


 Mhandisi  na kaimu meneja wa mamlaka ya mawasiliano ya simu (TTCL) George Mtikila akipokea hundi hiyo  kwa mkurugenzi wa hospitali ya rufaa dr Eliuter Samnkey kwa ajili ya kuleta vifaa hivyo na kufunga katika hospitali hiyo ya rufaa Mbeya

ZAIDI  ya shilingi million 15 zimetolewa na mamlaka ya mawasiliano Tanzanzania (TCRA)  nyanda za juu kusini   ajiri ya  kuboresha mfumo  mpya wa utoaji  huduma za matibabu kwa njia ya mawasiliano (TELE MEDICINE) ili kupunguza vifo na  gharama za usafiri kwa wagonjwa.

Mkurugenzi  Mkuu wa Hosptal ya Rufaa jijini Mbeya Eleuter Samky alishukuru mamlaka hiyo na kueleza kuwa mfumo huo utaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa   kupunguza  vifo na jamii kupatiwa huduma bora licha kuwepo na changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa.
“Mfumo huu utatusaidia sana na kuweza kuokoa maisha ya watanzania kwani kutakuwepo na mawasiliano mazuri na kuelimishana njia mbalimbali za kuweza kutoa matibabu kwa wagonjwa wetu hususan magonjwa ya watoto  na mgonjwa sugu yaliyoshindikana kutibika“Alisema.

Mhandisi  na kaimu meneja wa shirika la simu (TTCL) George Mtikila alisema kuwa  mkataba huo  wameingia na mamlaka ya mawasiliano (TCRA) utaanza kutumika kwa wakati na kwamba  lengo kuu ni kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa  katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zaidi.

Jengo la TTCL Mbeya
Mitambo ya kisasa ya mkonge wa taifa
Hudi iliyokabidhiwa leo
Moja ya wataalam wa mkonge wa taifa Humphrey Ngowi akiwaeleza waandishi wa habari jinsi mtambo huo unavyofanya kazi.

 HIVI NI KWELI HUDUMA ZOTE KWA WAJAWAZITO HUTOLEWA BURE? MAANA KUNA BAADHI YA HOSPITALI KUBWA HAPA JIJINI MBEYA MPAKA SASA WAJAWAZITO WANAKUJA NA VIFAA VYAO

 

HII NDIYO HALI HALISI MBEYA YETU IMEIKUTA KATIKA HOSPITALI KUBWA SANA HAPA MKOANI MBEYA KWENYE WODI YA WAMAMA WAJAWAZITO WALIOFANYIWA UPASUAJI HUAMBIWA WAKANUNUE DAWA NA VIFAA VINGINE VYA MATIBABUHUKU UKUTANI KUMEBADIKWA TANGAZO LA KUWA HUDUMA KWA WAJAWAZITO NI BURE PICHA HIYO INAJIELEZA JAMAA KATOKA KUNUNUA DAWA ZA KUMUHUDUMIA MKE WAKE ALIYEFANYIWA UPASUAJI HOSPITALINI HAPO MBEYA YETU INAENDELEA KUFUATILIA MATUKIO HAYO TUTAZIDI KUWAJULISHA.

Shirika lisilo la kiserikali la Jamhuri ya Czech BEZ MAMY limeanza kampeni ya kukusanya pesa Ulaya kwa ajili ya Kusaidia watoto yatima nchini Tanzania hasa mkoani Mbeya

Mratibu wa miradi na Mwakilishi wa Bez Mamy Africa Bw Chris Zacharia akiwa na wadau wa Czech BEZ MAMY 
Michoro ya picha za tingatinga inayotumika kukusanya michango hiyo
Mratibu wa miradi na Mwakilishi wa Bez Mamy Africa Bw Chris Zacharia akiendesha moja ya semina za kuchangia mfuko huo

Shirika lisilo la kiserikali la Jamhuri ya Czech BEZ MAMY limeanza kampeni ya kukusanya pesa Ulaya kwa ajili ya Kusaidia watoto yatima nchini Tanzania hasa mkoani Mbeya
Bez Mamy kwa kushirikiana na shirika la Kitanzania la jiji Mbeya Without Mother Organization kwa pamoja wamedhamiria kuinua elimu mkoani Mbeya kwa kusaidia ukarabati na utoaji wa misaada kwa shule za msingi jijini Mbeya, Ujenzi wa vituo vya watoto yatima, kuwalipia ada watoto yatima na kuboresha huduma za Afya jijini na wilaya mbalimbali za mkoa wa Mbeya
Akiongea na blog hii Mratibu wa miradi na Mwakilishi wa Bez Mamy Africa Bw Chris Zacharia alisema, wanatumia njia mbalimbali kukusanya pesa  hizo ambazo zitatumika katika ujenzi wa Bweni la wasichana katika kituo cha watoto yatima Mahango,Mswiswi pamoja na ujenzi wa Sekondari ya Ufundi katika Kijiji hicho cha Mahango
Njia zinazotumika kukusanya pesa hizo ni uuzaji wa michoro ya Tinga Tinga katika sehemu Mbalimbali nchini Slovakia na Jamhuri ya Czech na pia kupitia mtandao www.tingatingashop.cz
Njia nyingine ni utoaji wa Mihadhari katika vyuo vikuu, shule za sekondari za ufundi, Makanisani na kwa watu binafsi katika nchi hizo
Akizungumzia misaada na miradi hii bwa Chris Zacharia alisema,Ikiwa watu wa Ulaya wanajitoa kusaidia watoto wa afrika itawatia moyo zaidi kusaidia ikiwa watasikia watanzania wengine wenye uwezo pamoja na serikali wanajitoa kusaidia kundeleza miradi hii ambayo ina msaada mkubwa kwa uchumi na maendeleo ya nchi yetu

SOKO LA MWANJELWA MBEYA LAFIKIA ASILIMIA 80 YA UJENZI

SOKO KUU LA MWANJELWA LINALOENDELEA KUJENGWA MPAKA SASA LIMEFIKIA ASILIMIA 80 ILI KUKAMILIKA NA KUANZA KUFANYA KAZI
WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA WANAPATA MAELEKEZO YA HATUA ILIPOFIKIA YA UJENZI NA NINI KILICHOBAKI ILI JENGO LIANZE KUFANYA KAZI
HILI NI JENGO LA KUHIFADHIA TAKA SOKONI HAPO KABLA YA KUPELEKWA DAMPO



JENGO LA SOKO LA MWANJELWA LILIANZA KUJENGWA 25.02.2010  HADI SASA LIMEFIKIA HATUA YA UMALIZIAJI JAPO LIMECHELEWA KUKAMILIKA NA HATUA ZILIZOPO SASA KUFUATANA NA MKATABA WA UJENZI WA SOKO HILO NI KUWA MKANDALASI ANAKATWA TSH MILION KUMI KILA SIKU KWA MIEZI MITATU ALIYOPEWA AMALIZER NA KUKABIDHI JENGO LIKIWA LIMEKAMIRIKA.

ZIARA YA WAANDISHI WA HABARI ILILENGA KUJIONEA UJENZI UNAVYOENDELEA NA KUJUA KWA NINI JENGO LIMECHELEWESHWA KUMARIZIKA NA HATUA GANI ZIMECHUKULIWA ILI KUKAMILISHA JENGO HILO AMBALO LINA UWEZO WA KUWA NA VYUMBA VYA BIASHARA 450, STOR 3 KWA AJILI YA KUTUNZIA VITU, OFISI MBALIMBALI, POLISI POST MOJA, HOTEL 4, MADUKA MAKUBWA  WATAGAWA KWA MITA, MABUCHA 10, SEHEM YA WAFANYA BIASHARA WADOGO 444, SEHEM YA KUPAKI GALI 150, SEHEM YA KUHIFADHIA TAKA, MAJI SAFI, MAJI TAKA, GENERETA KUBWA, VYOO KWA AJILI YA WAHITAJI MAALUM NA VYA KAWAIDA KATIKA KILA GHOROFA. JENGO LITAKUWA NA GHOROFA 3.
HADI HATUA HII YA ASILIMIA 80 JENGO LIMEGHARIM TSH BILION 8.8 NA HADI UKAMINIKA LITAGHARIMU TSH BILION 13.
Picha na taarifa zote kwa hisani ya Mbeya Yetu.

Tuesday, November 27, 2012

MTOTO ALIYECHOMWA MKONO NA HATIMAE KUKATWA MKONO WAKE WA KUSHOTO ALETWA MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI

MTOTO ANETH KATIKATI NA MAMA YAKE KULIA WAKIINGIA ENEO LA MAHAKAMANI LEO

WILVINA MKANDALA ANAETUHUMIWA KWA KUMUUNGUZA NA KUSABABISHA KUKATWA KWA MKONO WA MTOTO ANETH AKIINGIZWA MAHAKAMANI HUKU AKIWA HATAKI KABISA KUPIGWA PICHA
WAKAZI WENGI WA JIJI LA MBEYA NA VITONGOJI VYAKE WAMEJITOKEZA KWA WINGI KUJA SIKILIZA KESI HIYO

MTOTO ANETH AKISALIMIANA NA MAMA ALIYEMUHUDUMIA HOSPITALINI KABLA YA MAMA YAKE MZAZI KUJA TOKA BUKOBA
MAMA ANETH AKIONDOKA NA MWANAE MARA BAADA YA HAKIMU KUMUONA MTOTO HUYO NA KUPATA MAELEZO MAFUPI TOKA KWA MTOTO ANETH AMBAE ALISHINDWA KABISA KUONGEA MARA TU ALIPO MUONA SHANGAZI YAKE HUYO ALIYEMCHOMA MOTO AKIINGIA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA KESI HIYO IMEAIRISHWA MPAKA TAREHE 6/12 / 2012
MTOTO ANETH MARA TU BAADA YA KUTOKA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKAMA AKISUBIRI KURUDISHWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA KUENDELEA NA MATIBABU
HUKU AKINA MAMA WAKIWA NA JAZBA YA KUTAKA HAKIMU AWAACHIE KIDOGO JAPO KWA DAKIKA TANO WAMFUNZE ADABU MTUHUMIWA HUYO KWANI WANADAI AMEWADHALILISHA SANA KWA KITE

Mwanamke anayetuhumiwa kumtesa kumlisha kinyesi na kumchoma moto mtoto wa kaka yake kumfungia ndani, amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika mahakama ya Wilaya ya Mbeya kujibu shtaka linalomkabili.

Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24)
Hataki kabisa kuonyesha sura yake

Aneth akiwa na wazazi wake mahakamani jana
Akirudishwa tena rumande mpaka tena tarehe 27/11

Baadhi ya akina mama wakiwa nje ya mahamaka wakisubiria kumwona mama huyo mwenye roho mbaya
Akina mama hao wakiwa na hasira kali walisikika wakisema tuachieni kidogo tumfunze adabu


MWANAMKE
anayetuhumiwa kumtesa kumlisha kinyesi na kumchoma moto  mtoto wa kaka  yake  kumfungia ndani,  amepandishwa    kizimbani kwa mara ya pili    katika mahakama ya Wilaya ya Mbeya kujibu
shtaka linalomkabili.
Mwendesha
mashtaka wa Serikali, Achiles Mulisa ameileza  Mahakama kuwa Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24)
Mkazi wa Majengo jijini humo  alitenda kosa la kusababisha majeraha akiwa
na nia ovu ambayo imemsababishia ulemavu mtoto  Aneth Gasto (4).
Mulisa
akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo Gilbert
Ndeuruo amesema kosa hilo ni kinyume cha kanuni ya adhabu kifungu  cha
222(a) sura ya 16 kama ilivyorejewa mwaka 2002.
 Kutokana na hali hiyo
mwendasha mashitaka huyo ameileza mahakama kuwa kesi inayo mkabili mwanamke
huyo ilihitaji mashahidi sita   ambao ni Dactari aliye mfanyia upasuaji mtoto
huyo   mwenyekiti wa Mtaa na barozi wake pamoja na Askari
mpelelezi wa kesi hiyo na mtoto mwenye .
 
Amesema
teyari mashahidi wanne kati ya sita wamekwisha toa ushahidi wao mahakani hapo .
Kutokana
na kosa hilo mshtakiwa amekana shitaka hilo ambapo alirudishwa mahabusu hadi
Novemba 27 Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Amesema
upande wa Jamhuri unamashahidi wanne ambao watatu kati yao teyari wamekwsha toa
ushahidi wao katika mahakama hiyo .
  
Amewataja
mashahidi hao kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Shuku Mwakanyamale, Daktari
anayemtibu mhanga katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya Dr. Paul Kasubi  na Habiba Mwakanyamale .
Wengine
ni Askari Polisi aliyepeleza kesi hiyo WP Pudensia na Mtoto mwenyewe  ambao wako tayari kufika mahakamani na kutoa
ushahidi wao mbele ya mahakama.
Awali
mshatakiwqa huyo aliieleza mahakama kuwa na uhusiano na mtoto  huyo ambapo
pia alikiri kuwa na taarifa za kile kinachoendelea juu ya matibabu ya mtoto huyo
na kuhusu kukatwa kwa mkono wake wa kushoto na kufungwa bandeji ngumu(POP)
kwenye mkono uliobaki.
Picha zote kwa hisani ya Mbeya yetu

Friday, November 23, 2012

Swali tete-Watoto Yatima wanauliza je mwaka 2012 nani atawalisha chakula cha sikukuu ya Christimas???

Kwa niaba ya Asasi isiyo ya kiserikali (CHIPRO) ninapenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa Vodacom/Vodacom Foundation kwa kuandaa chakula cha mchana, vifaa vya shule na vyakula mbalimbali ( Christmas 2011) kwa  watoto yatima na watoto waishio mazingira hatarishi 500, watoto hawa walitoka katika asasi mbalimbali  zilizopo jijini Mbeya.
Watoto na walezi wao walifurahi sana sana!

Watoto na walezi hawa wamekuwa wakiniuliza je mwaka 2012 tutakula, kunywa na kufurahi pamoja kama mwaka 2011??????  Sina jibu la kuwapa mpaka sasa, Ninamwachia Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma atatenda miujiza yake!!! 

Hivyo basi endapo utakuwa umeguswa na ombi la watoto hawa tafadhali wasiliana nasi kwa simu 0754301830.     Ubarikiwe sana!

Watoto na wageni waalikwa  wakiburudika kabla mgeni rasmi hajafika
Hapo chachaaaaa!!!!! (Ni furaha iliyoje!!! (FURAHA YAKO NINI??????)
Muandaaji wa shughuli bwana Mkama akizungumza na watoto /wageni waalikwa
Aliyekuwa Meneja wa Vodacom mkoa wa Mbeya bwana Kiswaga  akiongea maneno mafupi kumkaribisha mgeni rasmi (aliyekuwa mkuu wa Wilaya bwana E. Balama)
Afisa Maendeleo ya Jamii, mkoa wa Mbeya
Mmoja wa Kiongozi  wa asasi akisoma risala kwa mgeni rasmi
Mgeni rasmi Akiwasalimia na kuzungumza machache, baada ya kupokea risala
Muda wa maakuli ulifika, wafanyakazi wa Vodacom ndio waliotoa huduma ya chakula  kwa watoto
Huduma cha chakula zikiendelea
 


Hawa ni watoto yatima, na baadhi wameokotwa baada ya kuachwa na wazazi/mzazi,  umri wao ni kuanzia miaka 0-4, ambao wanalelewa na moja ya Asasi zilizoko mkoani Mbeya (Wanahitaji walezi), kama umeguswa unaweza kumchukua mtoto mmoja kwa makubaliano na asasi husika.
Bwana Poyo akiwa ameongozoana na kiongozi wa asasi mjawapo
Bwana Mwakifulefule akitoa huduma kwa watoto hao
Watoto wakiendelea kupata chakula cha mchana
Bwana Kiswaga akitoa huduma kwa watoto hawa
Bi Grace Lyon akiwa amembeba kichanga kilichookotwa wiki moja kabla ya tukio
Bi Zahra M. Mansour,  na wadau wengine wakiendelea kutoa huduma kwa watoto

Mzazi utamjua tu!!!

Mzazi utamjua tu!!!, watoto wamefurahi!!





Bwana Mramba hakuwa nyuma pia kutoa huduma kwa watoto
Waandaji wa shughuli wakiteta jambo (Bwana Mkama na bi Zahra)
Bwana Kapinga nae alikuwepo

Huduma zikiendelea kutolewa




Walezi  na viongozi wa Asasi mbalimbali











Muda wa zawadi huuooo!!!!!!!!!!!!!!! Watoto na vikundi vilivyohudhuria vilipewa zawadi zao





























Mmoja wa washiriki wa Asasi wakimshukuru dada Grace Lyon kwa niaba ya kampuni ya simu ya VODACOM/ VODACOM FOUNDATION
Mgeni rasmi akiondoka baada ya kumaliza sherehe

Kwa niaba ya baadhi Asasi zisizo za Kiserikali (CHIPRO), mkoa wa Mbeya, tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kampuni ya simu ya VODACOM/VODACOM FOUNDATION, kwa  chakula cha mchana , vifaa vya shule, na vyakula mbalimbali, kwa watoto waishio mazingira magumu na yatima katika mkoa wa Mbeya.

Nitakuwa mkosefu wa fadhila endapo sitatoa shukrani zangu za pekee kwa dada Grace Lyon, bwana Yessaya Mwakifulefule, bwana Mkama na wengineo wote waliosaidiana nasi kufanikisha shughuli hii.

Pia napenda kumshukuru bwana E. Balama kwa kukubali kushirikiana nasi! Mwenyezi Mungu awabariki sana!