Saturday, September 22, 2012

JUA MAANA YA HERUFI YA MWANZO YA JINA LAKO,


HERUFI A
Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. 

HERUFI B
wenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. 

HERUFI C
Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano.

HERUFI D
Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. 

HERUFI E
Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. 

HERUFI F
Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. 

HERUFI G
Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu.

HERUFI H
Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. 

HERUFI I
Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. 

HERUFI J
Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. 

HERUFI K
 Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. 

HERUFI L
Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. 

HERUFI M
Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. 

HERUFI N
Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. 

HERUFI O
Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia.

HERUFI P
Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu.

HERUFI Q
Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana.

HERUFI R 
Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani.

HERUFI S
Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa.

HERUFI T
Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika.

HERUFI U
Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi.

HERUFI V
Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika.

HERUFI W
Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari.

HERUFI X 
Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu.

HERUFI Y (YASINTA)
Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha.

HERUFI Z
Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo.
 

Wednesday, September 19, 2012

Shukurani

Nawashukuru wote wanaonipa moyo, hasa kwa hatua niliyochukua ya kuweza kupunguza/kutibu maradhi mbalimbali yanayowakabili watanzania wenzangu.

Ninaheshimu na kutunza siri za wagonjwa wangu, kwani heshima na utu wa mtu ni bora kuliko tiba.

Pia napenda kuwapa moyo wale wote wanaoumwa na kukata tamaa, kwani kuugua siyo kufa. 

Unatakiwa kufanya yafuatayo:- 

  1. Kuukubali ugonjwa unaokusumbua 

  2. Kutafuta suluhu ya tatizo(ugonjwa)

  3. Kupima ilikujua afya yako 

  4. Kula vyakula bora

  5. Kujipenda, kujithamini na kukubali changamoto aliyonayo!

  6. Kufanya mazoezi

  7. Kuwa muwazi kwa familia yako

    Kupata tiba 

    Nakaribisha wote wenye matatizo ya afya, wanahitaji ushauri, au wana mawazo, matangazo, mbalimbali  waweze kuwasiliana nami kupitia mtandao wangu.

    zaharam2012.blogspot.com/zaharam2012@gmail.com au simu namba 0754301830.

    wenu, 

    Zahra Mansour.

Saturday, September 15, 2012

KUTANA NA MWANA DADA MTAALAM WA MAGONJWA MBALIMBALI

 Zahra Mansour ambaye ni Mjasiliamali na tabibu wa magonjwa mbali mbali.



Zahra Mansour ni mwanamke anayetibu magonjwa mbali mbali anayepatikana Soweto Jijini Mbeya hivyo anawakaribisha wenye magonjwa kwa gharama nafuu kabisa.

Hata hivyo waliojaribu kutumia dawa zake wamepona na kutoa ushuhuda jinsi dawa hizo zinavyofanya kazi haraka na kwa uhakika.

Pia ili kukufikia ulipo Mwadada huyo huzunguka maeneo mbali mbali hasa minadani kwa ajili ya kukutana na wananchi wengi wenye matatizo na wanaohitaji matibabu.

Kwa sasa anaendelea na utafiti wa dawa ya kuponya maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi ambapo baada ya muda mfupi atawatangazia wananchi wote.

Moja ya magonjwa anayotibu ni Vidonda aina zote, Fungus,Kuongeza kinga Mwilini, Vidonda vya tumbo na mengine mengi ambapo hutumia dawa za miti shamba na vyakula ambavyo vimethibitishwa na mamlaka zinazohusika.

Nyote mnakaribishwa. na kwa taarifa zaidi endelea kutembelea mtandao huu wa www.zaharam2012.blogspot.com au kama una maoni tuma kupitia simu namba 0754301830 na email zaharam2012@gmail.com