Thursday, October 18, 2012

Salamu za Pole kwa familia ya mzee Mwihomeke wa Block T,Mbeya baada ya kufiwa na mke wake mpendwa Martha Mwihomeke.

Tarehe 07/10/2012 ilikuwa siku ya huzuni sana kwangu na familia yangu, hasa baada ya kuondokewa na mama yangu mpendwa (Mama Martha) ambaye nilifanya nae kazi (WRP) kwa kipindi cha miaka 7. Alikuwa ni mama ambaye aliniheshimu, kunifariji, kunishauri nk. , alikuwa ni mama ambaye ni  mchapa kazi, na mwenye moyo wa kujifunza na kujitolea ! She was a real model mother!

Kwa niaba ya familia yangu, ninapenda kutoa pole kwa familia ya bwana Mwihomeke wa Block T, Mbeya kwa kufiwa na mke (mama Martha Mwihomeke)

Pia napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa madaktari na wafanyakazi wote waliomuuguza hasa hospitali ya Rufaa,Mbeya.
Kwani Mungu alimpenda zaidi.

Mwenyezi Mungu apumzishe roho yake mahali pema peponi:AMINA!
Picha zote kwa hisani ya Joel Jailos,Mbeya

 
 
























Mume wa marehemu (mzee Mwihomeke) akitoa salamu za shukurani kwa ndugu jamaa na marafiki