LIVE !! MAHAFARI YA TANO YA CHUO KIKUU CHA TEKU MBEYA, WAHITIMU WAKIWA KATIKA MAANDAMANO KUELEKEA CHUO.
BENDI IKIWA INAWASINDIKIZA HAHITIMU
KILA MTU ANA FURAHA SASA KAMA WANAVYO ONEKANA
MEDIA NAO HAWAPO NYUMA KUCHUKUA MATUKIO YA MOJA KWA MOJA
WOTE WAKIWA WENYE NYUSO ZA FURAHA MUDA HUU
WAHITIMU MBALIMBALI WAKIWA WANAELEKEA CHUONI SASA
MDAU MKUBWA WA MBEYA YETU, FRANK PESS AKIWA NA JOHO LAKE KUELEKEA KATIKA MAHAFARI
HAPA MAANDAMANO YANAENDELEA
BREAKING NEWSSS WATOTO WAWILI WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI IMEZU INYALA MBEYA WAGONGWA NA ROLI NA KUFARIKI PAPO HAPO
Watoto hao wamegongwa katika barabara kuu itokayo Zambia kwenda dsm maeneo ya imezu inyara wilaya ya mbeya vijijini |
Vijana wameshaanza kuweka mawe barabarani kuzuia magari yasipite na ukizingatia hii ndiyo barabara kuu ya magari yaendayo Malawi na zambia na mikoa ya jirani |
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 01/11/2012.
TUKIO
KAMILI: BASI LA ABOOD NAMBA T 545 AZE LA KUTOKEA DAR KWENDA TUNDUMA
LAPATA AJALI MAENEO YA SAE(MBILINYI) BAADA YA KUGONGANA NA KENTA LILILO
SABABISHA AJALI HIYO, MMOJA AFARIKI HAPO HAPO!
Hivi ndivyo basi La Abood lilivyo pata ajali baada ya kugongana na Kenta
Basi la Abood
Hivi ndivyo Basi Lilivyo Haribika
Haya ni mambaki ya Vioo vilivyo vunjika
Baadhi ya vitu vikiwa vimemwagika chini
Hili ni Scania ambalo lilikuwa likitokea Zambia
Dirisha likiwa limevunjika
Baadhi ya Abiria wakiwa wanapata maelekezo kutoka kwa polisi
Hapa ndipo basi la Abbod lilipo gonga
*********************
BASI
LA ABOOD LENYE USAJILI WA NAMBA T 545 AZE LIMEPATA AJALI MAENEO YA SAE
SEHEMU MAARUFU KWA JINA LA KWA MBILINYI LIKITOKEA DAR ES SALAAM
KUELEKEA TUNDUMA. AJALI HIYO IMETOKEA BAADA YA LORI LA MIZIGO AINA YA
SCANIA LIKIWA LIMETOKEA ZAMBIA KUELEKEA DAR WAKATI WA KUTAKA KUPISHANA
NA BASI HILO, NA NDIPO GARI AINA YA KENTA IKAJITOKEZA NA KUJICHOMEKA
BARABARANI NA KUSABABISHA AJALI HIYO.
KATIKA
AJALI HIYO MTU MMOJA AMBAYE ANAITWA CHALE KITELEKE AMBAYE PIA ALIKUWA
NDIYE KONDA WA BASI HILO AMEFARIKI PAPO HAPO, PAMOJA NA MAJERUHI NANE
AMBAO WAMEKIMBIZWA HOSPITALINI .
MPAKA TONE MEDIA LIVE GROUP AMBAO NI WAMILIKI WA MTANDAO HUU TUNATOKA ENEO LATUKIO HIZO NDIZO TAARIFA TUMEFANIKIWA KUZIPATA.
HABARI KAMILI ITAWAJIA KESHO BAADA YA KUPATA TAARIFA KUTOKA POLISI.
BREAKING NUUUZ JUST NOW: BASI LA ABOOD LAPATA AJALI ILIYO TOKANA NA KUGONGANA NA KENTA !
HABARI
ZA UHAKIKA ZILIZO TUFIKIA KATIKA MEZA YETU YA HABARI ZINASEMA KWAMBA
BASI LA ABOOD LIMEPATA AJALI MBAYA BAADA YA KUGONGANA NA KENTA MAENEO YA
SAE JIJINI MBEYA. TAARIFA ZA AWALI ZINADAI KUWA KUTOKANA NA AJALI HIYO
BAADHI YA ABILIA WAMEBANWA VIBAYA NA BASI HILO, PIA MPAKA SASA MVUA
KUBWA INAENDELEA KUNYESHA, TONE MEDIA LIVE GROUP WAPO NJIANI KUELEKEA
KATIKA TUKIO.
ENDELEA KUFUATILIA HAPA MBEYA YETU KWA TAARIFA ZAIDI
LIVE!! SAKATA LA UKOSEFU WA MAFUTA JIJINI MBEYA.. HALI NI TETE .. DALA DALA NI 1000 KITUO HADI KITUO
Foleni ya kutosha kuelekea kufuata mafuta
Boda nazo zinangoja mafuta hapa
Magari yakiwa yameongozana foleni kwa ajili ya kutaka mafuta
Barabara nyeupe watu wamepaki magari Majumbani kahuna mafuta
Daladala nazo shida , hizi ni baadhi ukipanda tuu kila kituo utalipia 1000
Hii Gari ya kwanza mwisho ni ya Mwandishi Mkuu wa Mbeya yetu nae yupo kwa foleni
MEMBE: HAKUNA MTU KUSEMA ZIWA LOTE NI LAKE.
WAZIRI MEMBE AKIWA KATUMBASONGWE.
Mhe.
Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa akiongea na wazee waishio Katumbasongwe, kando ya Ziwa Nyasa
ndani ya Wilayani Kyela, Mkoani Mbeya.
Wakazi wa Katumbasongwe walimiminika kwa wingi kumsikiliza Mhe. Membe.
Wazee
wa Katumbasongwe wakinyoosha mikono kujitambulisha umri wao wakati wa
Mkutano wao na Waziri Membe uliofanyika jana Wilayani Kyela, Mkoani
Mbeya. Waziri Membe alikuwa Mkoani humo kwa ziara ya siku mbili ambapo
alitembelea maeneo na makazi ya wananchi waishio ufukweni mwa Ziwa
Nyasa.
WAZIRI MEMBE AKIWA MATEMA
Waziri
Membe akiongea na wakazi wa Matema, Wilayani Kyela ambapo aliwasihi
waendelee na shughuli zao za kujiletea maendeleo. Aidha, Mhe. Membe
alisema Serikali inajitahidi kadri iwezavyo kutafuta suluhisho la
mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi.
Wakazi wa Matema, waishio katika ufukwe wa Ziwa Nyasa, Wilayani Kyela wakimsikiliza Waziri Membe alipowatembelea jana.
Waziri
Membe (hayupo pichani) pia alipata fursa ya kuongea na wazee wa Matema
ikiwa ni sehemu ya mwisho wa ziara yake ya siku mbili Mkoani Mbeya.
Katika mazungumzo yake na wazee hao, Waziri Membe aliwaeleza kuwa ziara
hii ni sehemu ya kukusanya ushahidi muhimu kutokana na maelezo ya
historia watakazochangia hususan tangu enzi ya ukoloni kuhusu Ziwa
Nyasa.
Na TAGIE DAISY MWAKAWAGO,Mbeya
“Hakuna
mtu kusema Ziwa lote ni lake,” alisema Waziri Bernard K. Membe (Mb),
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kuongeza kuwa
lazima kuwe na dhamana inayoonesha mipaka, kanuni na sheria ili kuondoa
wingu la shaka yoyote hususan kwa Taifa lolote na wananchi wake.
Aidha,
Waziri Membe aliongeza kuwa Serikali ina jukumu la kumaliza mgogoro wa
mpaka wa Ziwa Nyasa kati yake na Malawi, na jitihada muhimu zinafanyika
ili kuumaliza kwa amani na utulivu.
Waziri
Membe aliyasema hayo jana mjini Mbeya alipokuwa akizungumza na Kamati
ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya, ambayo hiko chini ya Uenyekiti wa
Mhe. Abbas Kandoro, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
Akiainisha
jitihada hizo, Mhe. Membe alisema kuwa Kamati ya Taifa inayojumuisha
timu ya wanasheria na wataalamu wa mipaka imeundwa kwa madhumuni ya
kutatua mgogoro huo na timu ya Malawi. Pia kuna timu ya Kikosi Kazi
chini ya Waziri Membe, ambayo jukumu lake ni kukusanya nyaraka na
kumbukumbu muhimu za mgogoro huo tangu miaka ya 1890 hadi leo.
Kwa
mujibu wa maelezo ya Waziri, baada ya Kikosi Kazi kumaliza kazi yake,
kitawasilisha rasmi nyaraka kwa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete na kwa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili hatua muhimu za Serikali zifanyiwe
kazi.
Aidha,
Mhe. Waziri alisema kuwa kuna umuhimu wa kutumia vyombo vingine ili
kusaidia kutatua tatizo hili kama vile Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za
Kusini mwa Afrika (SADC), Baraza la Uongozi wa Wakuu wa Afrika la SADC
(Leadership Forum – SADC), Umoja wa Afrika (AU) na ikiwezekana kuipeleka
kesi kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
Kwa
upande wake, Mhe. Kandoro alisema kuwa hali Mkoani Mbeya ni tulivu na
kwamba maisha yanaendelea vizuri. Alikanusha kuhusu taarifa zisizo za
kweli zilizotangazwa kwenye mitandao kwamba mabomu yamerushwa Mkoani
Mbeya hususan kwenye maeneo ya mpaka wa Ziwa Nyasa.
Aidha,
Mkuu wa Mkoa aligusia ukamatwaji wa wavuvi na mitumbwi kutoka Malawi
ambayo ilikuja ufukweni mwa Tanzania, na kusisitiza kuwa hatua muhimu
zilichukuliwa kwa kuzingatia na kuheshimu ujirani mwema.
Katika
ziara yake, Waziri Membe pia alitembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya
Kyela, Bibi Margareth Malenga, ambapo alipata taarifa kuhusu hali ya
ulinzi na usalama katika mipaka ya Ziwa Nyasa, pamoja na mahusiano kati
ya Wilaya ya Kyela na Wilaya ya Karonga nchini Malawi. Wilaya ya Kyela
iko mpakani mwa Wilaya ya Karonga nchini Malawi.
Akisoma
taarifa ya Wilaya yake, Bibi Malenga alisema “hali ya mipaka ni tulivu
na kueleza kuwa hivi karibuni, mnamo tarehe 11 Oktoba, 2012 walipata
ugeni wa Mhe. Mganda Chiume, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi na ujumbe
wake akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Karonga nchini humo.”
Kwa
mujibu wa Bibi Malenga, lengo la ziara ya Waziri Chiume lilikuwa ni
kukagua mpaka wa Ziwa Nyasa kwa upande wao lakini waliona ni vizuri waje
Wilayani Kyela kuona hali ya mahusiano ilivyo baina ya wananchi wa
upande wa Kyela na wale wa Karonga.
Akiendelea
na ziara yake, Waziri Membe pia alipata fursa ya kuongea na wazee
alipotembelea maeneo ya Katumbasongwe na Matema yaliyopo katika ufukwe
wa Ziwa Nyasa.
“Tumekuja
hapa kupata ushahidi wenu wa kihistoria tangu enzi ya ukoloni ambao
utazisaidia Kamati zilizoteuliwa kutatua mgogoro huu ili ziweze
kukusanya kumbukumbu na kufanya kazi ipasavyo,” alisema Waziri Membe.
Aidha,
Waziri Membe aliwahakikishia amani na utulivu wananchi wa Kyela, na
kusema kuwa “Serikali inajitahidi kadri iwezavyo kutatua mgogoro huu kwa
njia ya kidiplomasia na hata kama ikiwezekana kwenda ICJ.”
Aidha,
Mhe. Membe kabla ya kumaliza ziara yake ya siku mbili Mkoani Mbeya
jana, pia alitembelea mipaka ya Kasumulu Katumbasongwe na Matema kwenye
ufukwe wa Ziwa Nyasa, katika Wilaya ya Kyela ambapo alizungumza kwa kina
na
Picha na maelezo, ni kutoka kwa Jose Mwaisango wa Mbeya Yetu Blogspot .
Abarikiwe sana kwa kazi zake!
Abarikiwe sana kwa kazi zake!
No comments:
Post a Comment